Mtokambali:Taifa bila maono haliwezi kuendelea katika Nyanja za uchumi.
Kiongozi
wa madhehebu ya TAG nchini amesema, taifa lolote haliwezi kuendelea kama
viongozi wake hawana maono ambayo yataleta mabadiliko ya kimaendeleo katika
nyanja zote zikiwemo za kiuchumi, elimu, afya na miundombinu ya barabara kwa
ajili ya kuwahudumia wananchi wake.
Kiongozi
huyo makamu wa rais wa makanisa ya TAG kanda ya AFRIKA, ambaye pia ni askofu
mkuu wa kanisa hilo hapa nchini, askofu Dkt. Barnabas Mtokambali katika ibada
ya uzinduzi wa jimbo la Tabora kasikazini na kusimikwa kwa askofu mpya wa jimbo
hilo ambapo amesema, mafanikio ya serikali ya awamu ya tano yanatokana na maono
ya mbali ya rais Dkt, John Pombe Magufuli.
Aidha
mgeni rasmi katika ibada hiyo mkuu wa wilaya ya Nzega, akitoa rai kwa viongozi
wa madhehebu ya dini amesema kuwa wilaya ya Nzega inakabiliwa na changamoto ya
mauaji ya ya kikatili hivyo ni fursa kwa viongozi kujikita vijijini ambapo
inaonyesha imani za dini bado ni duni.
Kwa
upande wake askofu mteule wa jimbo hilo, Mhashamu Endrew Kayamba amesema kuwa,
jukumu kubwa la kanisa ni kuwafikia watu wengi vijijini ambapo kuna uelewa duni
wa kumjua Mungu na kuthaminiana jambo ambalo husababisha uasi.
Comments
Post a Comment